• Kumekucha characters

UTANGULIZI

long-imgKumekucha ni mchezo wa radio utakaozinduliwa July 25, ukitazama mchango wa wanawake na vijana katika kutokomeza tatizo la uhaba wa chakula nchini Tanzania.

 

Mchezo wa Kumekucha ni wa kila wiki ambapo unaangazia maisha, vikwazo, na fursa za wakulima wa Tanzania. Mchezo utaanza kurushwa hewani July 25, nchi nzima. Mchezo utaruka hewani kila wiki mara moja kupitia Radio Free Africa (Taifa), Abood FM (Morogoro), Ebony FM (Iringa) and Bomba FM (Mbeya).

 

Wasanii wakubwa wa Bongo Movie kama vile JB, wachekeshaji Mau na Monica Sizya, na pia wanamuziki maarufu ‘JFK’ John Kitime na Mataluma, wamo katika mchezo huu uliochezewa katika maeneo ya mashambani nchini Tanzania.

 

Mchezo wa Kumekucha ika korido ya SAGCOT. Mchezo huu utaangazia zaidi juhudi za wanawake na vijana katika kilimo.

 

Sekta ya kilimo ni moja ya sekta muhimu katika uchumi wa Tanzania, inachangia 25% ya pato la taifa na 25% ya mazao yanaoyouzwa nje ya nchi. Kilimo kinaajiri Watanzania kwa asilimia 75, wengi wao wakiwa ni wanawake na vijana.

 

Wakati wanawake wakiwa ndio sehemu kubwa ya uzalishaji wa chakula hapa Tanzania, wengi wao hawana sauti katika maamuuzi yanayofanyika katika ngazi ya familia, hasa kwenye mgawanyo na matumizi ya mazao ya jasho lao.

 

Sheria na tamaduni zilizopo zinakwaza juhudi za wanawake kupata fursa za kiuchumi kwa sababu hawana haki ya kumiliki ardhi, au vifaa bora vya kilimo, vyanzo endelevu vya maji, ukosefu wa mikopo ambayo wanahitaji ili kufanikisha juhudi zao. Vikwazo hivi vinawazuia wanawake kujikwamua na umasikini, kupatia lishe bora familia zao, na pia kufikia malengo yao ya kuwa wakulima wa kisasa.

 

Behind the scenes Kumekucha TunuVivyohivyo, vijana nao wanawakilisha theluthi tatu ya waajiriwa wote katika sekta ya kilimo, lakini mara nyingi ajira zao ni za muda mfupi au vibarua, wanaotegemea kudra za majira na mikataba isiyo na manufaa yeyote kwao.

 

Mchezo wa Kumechucha umeandaliwa na Africa Lead, kwa kushirikiana na Media For Development International (MFDI), na kufadhiliwa na U.S. Agency for International Development (USAID). Watayarishaji wa Kumekucha, MFDI, waliwahi pia kutayarisha mchezo mwingine wa radio wa Wahapahapa na pia mchezo wa runinga wa SiriyaMtungi. Mchezo huu umefadhiliwa na watu  kutoka Marekani (USAID) na nia yake hasa ni kupunguza uhaba wa vyakula vyenye virutubisho  hapa Tanzania. Tunafanya hivi kwa kuongeza fursa za kiuchumi –  hasa kwa wanawake na vijana –  katika sekta ya kilimo

 

Kumekucha umetayarishwa chini ya ushauri wa Tanzania Food and Nutrition Center (TFNC), Tanzania Horticultural Association (TAHA), ACDI VOCA – NAFAKA,  Land O Lakes, RUDI, MWANZO BORA, The Rice Council of Tanzania, Technoserve, ANSAF (Non State Action Forum) na AMSHA (Youth in Agribusiness Forum).

 

RATIBA

Radio free africa logo
Mbeya (88.8 MHZ), Dodoma (89.0 MHZ), Dar es Salaam (89.3 MHZ), Iringa/Njombe (89.9 MHZ), Morogoro (93.8 MHZ)

Tuesdays: 10:30 – 11 am
Saturdays: 10:30 – 11 am

Ebony FM logo
Iringa (87.8), Njombe (88.2), Mbeya (94.7), Dar es Salaam (106.9)
Saturdays: 6 – 6:30 pm
Sundays: 6 – 6:30 pm

Bomba FM Logo
Mbeya (104.0 FM)
Mondays: 6:30 – 7 pm
Saturdays: 8 – 8:30 am

Abood FM logo
Dodoma (106.9 FM), Morogoro (89.9 FM), Dar es Salaam (101.7 FM)
Tuesdays: 6:30 – 7 pm
Wednesdays: 6:30 – 7 pm
Saturdays: 9:30 – 10 am

VIPINDI VYA REDIO

      EPISODE 01
      EPISODE 02
      EPISODE 03
      EPISODE 04
      EPISODE 05
      EPISODE 06
      EPISODE 07
      EPISODE 08
      EPISODE 09
      EPISODE 10
      EPISODE 11
      EPISODE 12
      EPISODE 13
      EPISODE 14
      EPISODE 15
      EPISODE 16
      EPISODE 17
      EPISODE 18
      EPISODE 19
      EPISODE 20
      EPISODE 21
      EPISODE 22
      EPISODE 23
      EPISODE 24
      EPISODE 25
      EPISODE 26
      EPISODE 27
      EPISODE 28
      EPISODE 29
      EPISODE 30
      EPISODE 31
      EPISODE 32
      EPISODE 33
      EPISODE 34
      EPISODE 35
      EPISODE 36
      EPISODE 37
      EPISODE 38
      EPISODE 39
      EPISODE 40
      EPISODE 41
      EPISODE 42
      EPISODE 43
      EPISODE 44
      EPISODE 45
      EPISODE 46
      EPISODE 47
      EPISODE 48
      EPISODE 49
      EPISODE 50
      EPISODE 51
      EPISODE 52

NYUMA ZA PAZIA YA MCHEZO WA REDIO

jb-recording2
writers producers kitime

HADITHI ZA KUMEKUCHA: FATUMA

Mama ni mkulima. Baba ni mdudu mharibifu.

Mwanamke wa kijijini, mfuata desturi, siku zote amekuwa akihatarisha mwili na nafsi yake, bila thawabu au ahsante, kwa kulima shamba la mume wake, kulisha na kuhudumia familia yake. Anapambana na hali mbaya za hewa, wadudu waharibifu, na umaskini. Lakini pale Manyusi anapotumia vibaya mavuno yake ya thamani, na anapopanga mbinu ya kumuoza binti yao, Fatuma analazimika kupambana na mume wake.

 

 

 

 

HADITHI ZA KUMEKUCHA: TUNU

Filamu ya Kumekucha – Tunu (Zawadi) ni hadithi ya Mashoto, ambaye anafanya kazi kama kondakta wa daladala mjini. Maisha ya Mashoto mjini ni ya upambanaji. Dar es salaam in maisha ya anasa, na Mashoto anapenda hivyo. Hana muda wa kufikiri juu ya watu na maisha aliyoyaacha kijijini, mpaka anapopata taarifa ya msiba wa mama yake.

 

Anaporudi nyumbani kwa ajili ya msiba, huzuni ya kumpoteza mama yake inamfanya achanganyikiwe.  Anaamini ardhi imelaaniwa na hataki kusikia lolote kuhusu hiyo. Baba yake, Sanga anapoteza matumaini juu yake. Baada ya muda kidogo, anajikuta anafanya kazi na dalali mwenye dhuluma, Kidevu. Ni mapambano magumu kwa Mashoto, wakati anajitahidi kutafuta dhumuni ndani ya kijiji.

 

Lakini bado, mama yake amemuachia zawadi. Sauti yake, na uwepo wake usioonekana, sauti inayomuambia kwa upole afungue macho na kuzibua masikio yake, ili aweze kujifunza somo juu ya uoto wa asili wa dunia na mizizi itoayo rutuba kutoka kwenye hiyo.

 

Baada ya kufukuzwa nyumbani na baba yake kwa kutumia pesa kidogo alizoziacha mama yake, Mashoto  lazima ajifunze kuishi kwa kutegemea ardhi. Lazima ajifunze jinsi ya kukabiliana na maadui wa zamani na kutafuta marafiki wapya. Lazima ajifunze kupambana na kupenda. Lakini jambo la muhimu zaidi,   Mashoto lazima atambue kile anachokipigania.

ANGALIA FILAMU

Tunu

Fatuma

MATANGAZO

WASHIRIKI

logo-usaid
logo-feed-the-future
logo-africa-lead