Mwanajeshi, muamuzi na mfanyabiashara aliyeishiwa.
Mwamtitu anaamini kuwa mwanaume ndie kichwa cha nyumba na mtafutaji wa mkate wa kila siku. Anayo imani kuwa atafanikiwa kibiashara siku moja lakini ukweli ni kwamba hana nidhamu ya biashara na fedha kama alivyo mkewe. Anapata wakati mgumu kukubaliana na hali hii. Anapopata ajali na kulazwa hospitalini, maisha ya Mwamtitu yanaharibika kabisa. Je, atakuja kukubaliana na ukweli kwamba mkewe ni bora zaidhi yake katika biashara?